Thursday, April 6, 2017

NAPE KUWAELEZA UKWELI WOTE WAPIGA KURA WAKE WA MTAMA JUMAMOSI HII


ALIYEKUWA Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnuye amesema kuwa Jumamosi hii jimboni kwake Mtama mkoani Lindi, ataeleza UKWELI WOTE wa yaliyomtokea siku za hivi karibuni.
Nape ambaye aliondolewa kwenye nafasi hiyo wiki chache zilizopita baada ya kupokea taarifa ya Kamati ya Uchunguzi ya Saa 24 aliyoiunda kufuatia Kituo cha Clouds TV kuvamiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Nape aliahidi kupeleka ripoti hiyo kwa wakuu wake ambao ni Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Rais John Pombe Magufuli ambapo siku iliyofuata Rais alimteua aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Harrison Mwakyembe kuchukua nafasi ya Nape.
Aidha Nape Nnauye alimshukuru Rais Magufuli kwa kumteua Mwakyembe kwenye nafasi hiyo na kuahidi kuendelea kuipa ushirikiano serikali.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Nape ameandika;
“Shukrani kwa wote mlioniunga mkono katika kusimamia haki. Narudi Mtama kuwaeleza wapiga kura wangu UKWELI WOTE. Ni Jmosi tar 8/4/17” Nape

MSANII ROMA MKATOLIKI AVAMIWA STUDIO ZA TONGWE USIKU, AKAMATWA!

Taarifa iliyotolewa na Mbunge ambaye pia ni Rapa, Joseph Haule ‘ Prof. Jay’ kupitia ukurasa wake wa facebook imeeleza kuwa Rapa Ibrahim Mussa ‘ROMA Mkatoliki’ amevamiwa akiwa katika studio za Tongwe Records kisha kukamatwa na polisi ambao hawajafahamika mara moja.
“ROMA MKATOLIKI AMEKAMATWA USIKU HUU…
Nimestushwa sana kusikia kuwa kuna watu wamevamia studio za TONGWE RECORDS majira ya saa moja usiku na wamemchukua ROMA @roma2030 , MONY @moni_ centrozone na kijana wa Kazi na pia wamechukua COMPUTER ya studio na Screen (Tv) na wameondoka navyo kusikojulikana..
Mpaka sasa hatujui wamewapeleka wapi!!  Ameandika Prof. Jay.

Juhudi za kumtafuta ROMA tangu alfajiri hazijafanikiwa mpaka sasa kwani simu yake inaita bila kupokelewa.
Wadau wa muziki wamekuwa wakiuliza wakitaka kufahamu ROMA amekamatwa kwa kosa gani na amepelekwa kituo gani cha polisi jambo ambalo jeshi la polisi halijaeleza mapaka sasa.
Chanzo: Global Publishers

JINSI YA KUITAFUTA NGOZI NZURI KWA KUTUMIA MATUNDA


LEO nitaongelea suala zima la binadamu kuwa na ngozi nzuri na yenye mvuto ambayo utaipata kwa kunywa maji ya matunda. Kama tulivyozoea, maji ya kunywa huwa yanatajwa kwenye kuing’arisha ngozi na kuondoa sumu mwilini mwa binadamu, sasa leo nitakufundisha jinsi ya kunywa maji mengi zaidi ambapo utatumia na matunda ili kuipata ngozi iliyo nyororo.
Chukua jagi lenye maji safi ya kunywa, changanya na limao, ndimu na vipande viwili vya tango, vyote vikiwa na maganda yake. Yaani usimenye. Hapa nikiongelea matunda simaanishi juisi yake bali namaanisha vipande ambavyo havijakatwa vya matunda hayo.
Hatua ya kwanza ni kuchanganya na maji hayo, hatua ya pili ni kuweka kwenye friji au pembeni yake kwa muda wa saa nane ili kupata ile ladha, kisha kunywa. Faida ya maji hayo
Kwanza; yatakusaidia kunywa maji kwa urahisi kwani yatakuwa na harufu nzuri na ladha inayonyweka zaidi ya maji matupu.
Pili;  yatasaidia kupunguza tumbo kwa wale wasiopenda matumbo makubwa au jina rahisi vitambi. Tatu;  yatasaidia kukupa ngozi nyororo yenye kuteleza. Kama utakosa matunda hayo, unaweza kutumia zabibu, tikiti maji, chungwa na strawberry.
Chanzo: Gazeti Amani