Friday, December 2, 2022

WABUNGE WARUSHIANA ‘MAKONDE’ BUNGENI

 

Wabunge nchini Senegal wameingia katika sakata la kurushiana makonde na viti siku huku mmoja wao akimpiga kofi Mbunge wa kike usoni kutokana na mjadala wenye ukinzani kushamiri wakati wa kikao cha majadiliano Bungeni.

 

Hata hivyo, tukio hili linatokea wakati wa upigaji kura wa bajeti ya Wizara ya sheria ya mwaka ujao (2023), ukifanyika na uwasilishwaji wa bajeti ukiendelea huku Mbunge wa upinzani, Massata Samb alimpiga Amy Ndiaye Gniby wa muungano tawala wa Benno Bokk Yakaar (BBY).

 

Gniby alilipiza kwa kurusha kiti upande wa Samb kabla ya mbunge mwingine kumvuta hadi sakafuni na kupelekea kikao hicho kusitishwa lakini hata hivyo wabunge hao waliendelea kurushiana makonde na matusi.

 

Mzozo huo, ulitokea huku kukiwa na uhasama kati ya wanasiasa wa chama tawala na cha upinzani huku Wanaharakati wa wanawake na wanachama wa muungano unaotawala wakionesha kukerwa na shambulio la kimwili dhidi ya Ndiaye.

 

Wanaharakati hao, wamesema wataendesha kampeni ya uhamasishaji kuhusu unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana kwakua tukio hilo limechukua taswira mpya na kusambaa kote ulimwenguni kitu ambacho kinaweza kuleta athari na mkanganyiko.

 

Mvutano kati ya wanasiasa watawala na wa upinzani umekuwa ukiongezeka ambapo uchaguzi wa wabunge wa Julai, 2022 ulishuhudia chama tawala kikipoteza wingi wake wa kura kutokana na uwepo wa hofu kwamba Rais Macky Sall atawania muhula wa tatu mwaka wa 2024.


Source: Dar24 Blog

MABASI YOTE YA SHULE KUWA NA MAKONDAKTA WA KIKE - DKT. GWAJIMA

 

Serikali imeagiza mabasi yote yanayobeba wanafunzi kuwa na kondakta wa kike na mabasi yote yafungwe kamera maalum.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima ametoa agizo hilo alipokuwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe katika Shule ya Star LightPre and Primary School, ambapo mtoto wa miaka sita wa darasa la kwanza anadaiwa kubakwa na kondakta wa gari hilo.

Dkt. Gwajima amesema "watuhumiwa kwa sasa  wapo ndani na wameshapanda mahakamani, pongezi wote waliowajibika haraka kesi inaendelea," amesema Gwajima.

Aidha Dkt. Gwajima amesema ana uhakika kuwa suala hilo halitaleta shida kwa kuwa hakuna gharama yoyote itakayoongezeka kwa kuwa ni jinsia tu ndio inabadilika.  Hii itawezesha ulinzi imara kwa mtoto wa kwanza kuchukuliwa na wa mwisho kurejeshwa,”             

"Tunaangalia uwezekano huko mbele kuwe na haja ya kufunga kamera kwenye mabasi ya shule. Lazima wateja walindwe yaani mtoto ni mteja jamani inakuwaje analipia huduma alafu anafanyiwa vitendo vya kikatili?" aliongeza Waziri Gwajima.

Tamko hilo la Serikali linakuja ikiwa ni siku chache baada ya kusambaa kwa taarifa katika mitandao ya kijamii inayoelezea mtoto wa miaka sita kubakwa na dereva na kondakta wa basi la shule.

Source: Habari Leo instagram

Thursday, December 1, 2022

KUPATA MATOKEO YA DARASA LA SABA 2022 BONYEZA LINK HAPO CHINI

 https://matokeo.necta.go.tz/psle2022/psle.htm


BREAKING NEWS: NECTA YATANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA 2022

 

Kaimu Katibu Mtendaji wa NECTA, Athumani Amasi

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) leo Desemba 1, 2022 limetangaza matokeo ya darasa la saba kwa mwaka 2022 ambapo limetangaza kufuta matokeo yote ya Watahiniwa 2194 sawa na asilimia 0.16 ya Watahiniwa 1,350,881 waliofanya mtihani ambao wamebainika kufanya udanganyifu katika mtihani huo wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2022.

Kati ya hao wasichana ni 558,825 ambao ni sawa na asilimia 78.91 na wavulana ni 514,577 sawa na asilikia 80.41.

Kaimu Katibu Mtendaji wa Necta, Athumani Amasi ametangaza matokeo hayo leo Alhamisi Desemba Mosi, 2022 wakati akizungumza na wanahabari jijini hapa kuhusu mtihani huo wa kumaliza elimu ya msingi uliofanyika Oktoba 5 na 6 mwaka huu.

Almasi amesema katika matokeo ya mwaka 2021 watahiniwa walikuwa 907,802 sawa na asilimia 81.97.

Amesema kitakwimu kuna kupungua kwa ufaulu kwa asilimia 2.35 ingawa idadi ya watahiniwa waliofaulu imeongezeka kwa watahiniwa 165, 600 sawa na asilimia 18.24 ikilinganishwa na mwaka jana.

Ili kupata matokeo hayo ingia kwenye  link hii:   https://matokeo.necta.go.tz/psle2022/psle.htm

Source: Global Publishers

MWIMBAJI WA MAREKANI JAKE FLINT AFARIKI SAA CHACHE BAADA YA HARUSI

 

Marehemu Jake Flint enzi za uhai wake.


Hali ya sintofahamu inaendelea kutanda kuhusu kifo cha mwanamuziki wa taarabu nchini Marekani, Jake Flint, saa chache baada ya harusi yake siku ya Jumapili.

Flint, 37, alifariki usingizini huko Oklahoma, meneja wa zamani Brenda Cline alisema katika chapisho la mtandao wa kijamii.

Heshima zimeanza kumiminika kwa mwimbaji huyo ambaye alichukuliwa kuwa nyota anayechipukia katika muziki aina ya “Red Dirt”, aina ya muziki wa taarabu kutoka Oklahoma.

Mke mpya wa Flint, Brenda Wilson Flint, amechapisha video ya wawili hao wakicheza chini ya mti siku ya harusi yao.

“Tunapaswa kupitia picha za harusi lakini badala yake lazima nichague nguo za kumzika mume wangu,” aliandika ujumbe kwenye mtandao wa Facebook.

Wenzi hao walifunga ndoa katika sherehe huko Tulsa siku iliyotangulia.

“Kwa moyo uliovunjika na huzuni kubwa lazima nitangaze kwamba Jake Flint ameaga dunia,” meneja wa zamani Brenda Cline aliandika.

“Nimejaribu mara kadhaa leo kuweka ujumbe, lakini huwezi kutoa maoni juu ya kile ambacho huwezi kushughulikia.”

Mtangazaji wa muda mrefu Clif Doyal alithibitisha kifo hicho kwa gazeti la Oklahoman, akisema kwamba Flint alifariki usingizini.

“Sidhani kama nimewahi kukumbana na hali ya kushtua kama hii ya kupoteza mtu na jinsi hii ni ukatili kwa Brenda, mke

“Kuwa bibi na mjane katika masaa machache tu haiwezekani.”

Red Dirt, aina ya muziki wa taarabu, imepewa jina la rangi tofauti ya udongo katika jimbo la Oklahoma, ambapo Flint alizaliwa katika mji wa Holdenville kabla ya kuhamia Tulsa.

Source: Global Publishers

Monday, November 21, 2022

RAIS WA ZAMANI WA MAREKANI KUCHUNGUZWA

 

Wizara ya Sheria ya Marekani juzi ilimtaja mpelelezi wa zamani wa uhalifu wa kivita kama Wakili maalum wa kusimamia uchunguzi wa uhalifu dhidi ya Donald Trump, siku tatu baada ya Rais huyo wa zamani kutangaza kuwa atagombea tena uchaguzi wa Rais wa mwaka 2024.

Trump, ambaye anadai kuwa ‘anawindwa na wachawi’, alikashifu hatua hiyo akisema isiyo ya haki na siasa chafu katika nchi yao huku Ikulu ilikanusha uingiliaji wa kisiasa, lakini uchunguzi wa mawakili maalum wa Rais wa zamani na mgombea wa sasa unaweka mazingira ya vita vya kisheria.

Katika mkutano na waandishi wa habari, Mwanasheria Mkuu Merrick Garland alitangaza uteuzi wa Jack Smith, ambaye alikuwa mwendesha mashtaka mkuu huko The Hague, akichunguza uhalifu wa kivita wa Kosovo, kuchukua jukumu la chunguzi mbili zinazoendeshwa dhidi ya Trump.

Uchunguzi mmoja unaangazia juhudi za Rais huyo wa zamani za kutengua matokeo ya uchaguzi wa 2020 na shambulio la Januari 6, 2021 dhidi ya Ikulu ya Marekani lililofanywa na wafuasi wake.

Nyingine ni uchunguzi wa hifadhi ya nyaraka za siri za Serikali zilizonaswa wakati Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI) lilipovamia kwenye makazi ya Trump ya Mar-a-Lago huko Florida Agosti mwaka huu.

Mwanasheria Garland alisema kumtaja wakili maalum ni kwa manufaa ya umma kwa sababu Trump wa chama cha Republican na mrithi wake wa Chama cha Democratic, Joe Biden wameeleza nia yao ya kugombea 2024, ingawa ni Trump pekee ndiye ametangaza rasmi kwa sasa.

TRUMP AREJEA TWITTER

 Akaunti ya Twitter ya Rais wa Zamani wa Marekani, Donald Trump imerejeshwa na mmiliki wa kampuni hiyo na boss, Tesla Elon Musk, ambapo wafuasi wa mtandao huo wamepiga kura ya kurejesha akaunti hiyo.

Akaunti hiyo, ambayo ilifungiwa kufuatia shambulio la Januari 6, 2021, kwenye Capitol, imerejeshwa baada ya Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Twitter na mmiliki mpya kuhoji watumiaji wa Twitter ikiwa Trump anafaa kurejeshwa.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter Musk ameandika, “Watu wamezungumza. Trump atarejeshwa,” “Vox Populi, Vox Dei,” akaongeza kwa kilatini akimaanisha “Sauti ya watu ni sauti ya Mungu.”

Kwa mujibu wa kura zilizopigwa mpaka kufikia asubuhi ya Novemba 20, 2022 asilimia 51.8 ya kura milioni 15 zilizopigwa kwa siku mbili zilitaka Trump arejeshwe. Asilimia 48.2 ya kura hizo hawakutaka Trump arejee katika jukwaa hilo.

Uamuzi huo unaweka mazingira ya kurejea kwa Rais huyo wa zamani kwenye mtandao wa kijamii ambapo hapo awali alikuwa na ushawishi mkubwa zaidi, ikiwa ni mtumiaji mwenye utata.

 

Akiwa na karibu wafuasi milioni 90, tweets zake mara nyingi ziliweka mzunguko wa habari na kuendesha ajenda huko Washington.

Itakumbukuwa kuwa Trump alisema angesalia kwenye jukwaa lake, Truth Social, badala ya kujiunga tena na Twitter, lakini mabadiliko katika mtazamo wake yanaweza kuwa na athari kubwa za kisiasa.

Rais huyo wa zamani alitangaza mwezi huu kwamba atawania uteuzi wa urais wa Republican mwaka wa 2024, akilenga kuwa kamanda mkuu wa pili kuwahi kuchaguliwa kwa mihula miwili tofauti.


Source: dar24.com

Wednesday, March 30, 2022

TWO YOUNG COUSINS DIE WHILE PLAYING WITH GUN DURING LIVESTREAM

 

A pair of young cousins are both dead following what cops are calling a murder-suicide that was livestreamed at a St. Louis birthday party.

Kuaron Harvey, 14, and Paris Harvey, 12, were live on Instagram around 2 a.m. Friday when a gun that the younger child was playing with went off and killed her cousin — prompting her to shoot herself, CBS News reported.

Police initially described the deadly incident as a murder-suicide — but their family says it wasn’t so.

“It was no murder. It wasn’t a suicide,” Paris’ distraught mother, Shinise Harvey, told the St. Louis Post-Dispatch. “It was a freak accident. It happened.”

She said relatives who saw the video said the pair was “trying to be too hip” when the shooting happened.

Police told the outlet that the cousins were found unresponsive at 2:07 a.m. and both were later pronounced dead at the scene.

“It wasn’t a situation where they were arguing or anything like that,” said Susan Dyson, the dead girl’s grandmother. “They were playing with a gun when they shouldn’t have been. Of course, they shouldn’t have been doing it.

“I think it just went off,” Dyson said. “It went off by mistake.”

She said the two were at a birthday party for younger family members when they went into the bathroom to film in front of a mirror. That’s when the tragedy happened.

The family said the two were so close, they were like “brother and sister,” and typically horsed around when together, pulling pranks, rapping or making videos.

“No matter how good we raise our kids, they still are going to venture off,” Shinise Harvey told the Dispatch.

St. Louis police have not released the results of the department’s investigation.

Wednesday, August 4, 2021

TEENAGE GIRL DIES AFTER ‘PASSING OUT’ WHILE HAVING SEX IN CAR WITH OLDER MAN

Gabrielly smiling

A 15-year-old has tragically died after "passing out" while having sex with an older man in a car in Brazil.

 

Gabrielly Dickson Alves Nascimento was rushed to hospital on July 29 but died the next morning.

 

A unnamed 26-year-old man told the police the two had been having sex when the girl turned pale.

 

Doctors at the the UPA Jardim Casquiero medical facility in Cubatão, São Paulo, diagnosed her with a cardiopulmonary arrest and desperately tried to save the teen but she sadly died in the early hours of the following morning, the Daily Star reports.

 

Police are now awaiting the results of a post-mortem. There were, however, no other indications of a physical assault.

 

The man, described as a “general services assistant” is not believed to have been charged with any crime.

 

In Brazil, the age of sexual consent is 14.

 

Dickson's family was not aware of her relationship with the the man, according to local reports, and she was not thought to have been suffering from any pre-existing conditions.

 Gabrielly

“Forensic examinations were requested and the case registered as a suspicious death by the Cubatão Police Station,” the Cubatão Ministry said in a statement.

Dickson's sudden death sparked an immediate outpouring of grief among her friends, family and neighbours in the township of Cubatão, who paid their respects via social media.

 

The girl's friends and classmates described her as hard-working, dedicated, happy and loved by everyone.

 

Dickson’s final post on Twitter, published just two days before her untimely death, read “who is it that hates me?”

 Source: www.mirror.co.uk