Wednesday, October 17, 2018

MANENO YA MWAKASEGE WAKATI WA KUAGA MWILI WA MWANAE


Mchungaji na Mwalimu Christopher Mwakasege jana Jumanne Oktoba 16, 2018 aliongoza maombi ya ibada ya kuaga mwili wa mwanaye wa pekee wa kiume, Joshua Mwakasege. Ibada iliyofanyika  katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Mbezi Beach na kuhudhuriwa na mamia ya watu, akiwemo Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.

Akiongoza maombi hayo, Mwakasege alisema; “Kabla ya kifo, niliwasiliana na Joshua, nilimuahidi kuwa tungezungumza tena jioni baada ya kumaliza semina. Nilipomaliza semina nilimpigia simu lakini iliita bila kupokelewa. Baadaye mlinzi wa kazini kwao alipokea na akatueleza kuwa Joshua amekimbizwa hospitali,” amesema Mwakasege.

Joshua alifariki siku ya Alhamisi, 11 Oktoba 2018 baada ya kuugua ghafla akiwa ofisini kwake World Bank, Dar es Salaam ambapo aliwahishwa hospitali ya Aga Khan na kufariki baadae usiku huo.

 Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu Joshua. Amen.

No comments: