Wednesday, September 20, 2017

MAGUFULI AMMWAGIA SIFA MBUNGE WA CHADEMA

Rais John Pombe Magufuli ambaye leo Septemba 20, 2017 yupo kwenye ziara ya kikazi mkoani Manyara katika Wilaya ya Simanjiro amefunguka na kumsifia Mbunge wa Simanjiro James Ole Millya na kusema ni Mbunge mchapakazi.

Rais Magufuli amesema Ole Millya ni mchapakazi kutokana na ukweli kwamba Mbunge huyo amelelewa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kukulia ndani ya chama hicho hivyo sasa yupo CHADEMA lakini moyo wake ni CCM.

"Miliya ni mchapakazi, kwa sababu amelelewa na CCM, unaweza kumuona ni CHADEMA lakini moyo wake huyu ni Chama Cha Mapinduzi (CCM)" alisema Magufuli.

Mbali na hilo Rais Magufuli amesema kuwa Mungu huenda alikosea kuipa Tanzania madini ya Tanzanite kwani madini hayo yamekuwa yakiibiwa huku Watanzania wenyewe wakishindwa kunufaika na mapato ya madini hayo.

"Mungu alifanya makosa alileta Tanzanite kwa Watanzania, lakini kama hakufanya makosa basi tubadilike jinsi ya kutumia Tanzanite. Tanzanite ingekuwa inatumika vizuri kusikungekuwa na tatizo la barabara hapa Simanjiro, hapa Simanjiro msingekosa hata Ambulance moja lakini kwa kuwa hamna gari hata moja ya wagonjwa basi mimi nitaleta gari ya wagonjwa hapa nitajua nifanye nini, nitawakata kata huko tutapata gari" alisema Rais Magufuli.

No comments: