Friday, September 13, 2013

SHOGA (AUNT ASU) AOKOKA NA KUACHANA NA MAMBO YA KISHOGA

Aunt Asu enzi akiwa shoga.




Aliyekuwa shoga maarufu aliyekuwa akijulikana kwa jina la Anti Asu (sasa anaitwa Amos) ameokoka rasmi na kuachana kabisa na shughuli hiyo ambayo ni kinyume kabisa na maadili yetu ya kitanzania.

Aunt Asu alitangaza uamuzi wa kuachana na ushoga na kumrudia Mungu katika kipindi cha Mitikisiko ya  Pwani cha kituo cha Times FM ambapo huwa ni mahususi kwa kupiga nyimbo za taarabu na habari zinazuhusu wanamuziki wa taarab na wadau wa muziki huo hapa nchini na kinaendeshwa na mtangazaji huyo Dida Shaibu mwenye masham sham mengi katika kukichagiza.

Watu kadhaa wameonekana kutoa maoni yao tofauti wakimpongeza kwa hatua yake hiyo huku wengi wakisema ama kwa hakika Mungu mkubwa na inapaswa woote wenye  tabia kama alizoziacha Aunt Asu waache mara moja na kumrudia Mungu.

Katika picha zake zilizooneshwa katika mitandao mbalimbali, watu wengi walionekana kutotambua kama aunt Asu ni mwanamke au mwanaume kutokana na mavazi ya kike aliokuwa ameyavaa lakini picha nyingine zinazomuonesha akiwa amevalia suti yupo kanisani mara baada ya kutangaza kuokoka ndizo zimefanya watu waamini kuwa ni mwanaume.

Picha za chini zinamuonesha Aunt Asu baada ya kuokoka na kuachana na mambo ya kishoga.



Aunt Asu (mwenye suti) baada ya kuokoka na kutangaza kuachana na mambo ya kishoga.

No comments: