Thursday, December 1, 2022

BREAKING NEWS: NECTA YATANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA 2022

 

Kaimu Katibu Mtendaji wa NECTA, Athumani Amasi

Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) leo Desemba 1, 2022 limetangaza matokeo ya darasa la saba kwa mwaka 2022 ambapo limetangaza kufuta matokeo yote ya Watahiniwa 2194 sawa na asilimia 0.16 ya Watahiniwa 1,350,881 waliofanya mtihani ambao wamebainika kufanya udanganyifu katika mtihani huo wa kumaliza elimu ya msingi mwaka 2022.

Kati ya hao wasichana ni 558,825 ambao ni sawa na asilimia 78.91 na wavulana ni 514,577 sawa na asilikia 80.41.

Kaimu Katibu Mtendaji wa Necta, Athumani Amasi ametangaza matokeo hayo leo Alhamisi Desemba Mosi, 2022 wakati akizungumza na wanahabari jijini hapa kuhusu mtihani huo wa kumaliza elimu ya msingi uliofanyika Oktoba 5 na 6 mwaka huu.

Almasi amesema katika matokeo ya mwaka 2021 watahiniwa walikuwa 907,802 sawa na asilimia 81.97.

Amesema kitakwimu kuna kupungua kwa ufaulu kwa asilimia 2.35 ingawa idadi ya watahiniwa waliofaulu imeongezeka kwa watahiniwa 165, 600 sawa na asilimia 18.24 ikilinganishwa na mwaka jana.

Ili kupata matokeo hayo ingia kwenye  link hii:   https://matokeo.necta.go.tz/psle2022/psle.htm

Source: Global Publishers

No comments: