Thursday, October 18, 2018

MWANAFUNZI AUA WENZAKE 19 KWA RISASI, AJIUA



Wanafunzi 19 wamekufa na wengine makumi wamejeruhiwa baada ya mwanafunzi mwenzao kuwafyatulia risasi katika chuo cha eneo la Crimea nchini Urusi.

Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 18, anadaiwa kupita katika vyumba kadhaa vya bweni la wanafunzi pamoja na mgahawa wa chuo hicho akifyatua risasi hovyo.

Mshambuliaji huyo ambaye ametajwa kwa jina la Vladislav Roslyakov, alijiua baada ya kufanya mauaji hayo, kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na kamati maalum ya vyombo vya ulinzi vya Urusi.

Vyombo vya ulinzi na usalama vimeeleza kuwa mbali na shambulizi hilo pia milio ya milipuko kadhaa ilisikika katika eneo hilo. Wapelelezi wa tukio hilo wameeleza kuwa walibaini kuwepo kwa kilipuzi kimoja kwenye mfuko wa mshambuliaji huyo.

Taarifa za awali zililitaja tukio hilo kama shambulizi la kigaidi, lakini wapelelezi wa Urusi walieleza kuwa halikuwa na uhusiano na ugaidi.

No comments: