Wednesday, April 18, 2018

NDALICHAKO AJITETEA RIPOTI YA CAG - Angalia VIDEO

Image result for picha ya ndalichako
DODOMA.  Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe Prof. Joyce Ndalichako amesema anaitumia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali kama changamoto na chachu ya kuendelea kufanya kazi nzuri.

Ndalichako ameyasema hayo jana wakati akijibu hoja za ripoti ya CAG iliyosomwa wiki iliyopita bungeni.

Wiki iliyopita mawaziri wanane walifanya mkutano na waandishi wa habari wakijibu hoja za ripoti ya CAG.

"Serikali ya awamu ya tano kwenye suala la udhibiti haina utani, kila mtu ameona kazi ambayo imefanyika, tunapopata ripoti ya CAG, inatupa chachu ya kuendelea na kazi nzuri inayofanywa na serikali ya awamu ya tano," amesema.

Amesema kama CAG alivyoshauri, watafanyia kazi mapendekezo ya CAG na pia watawachukulia hatua watendaji wanaotumia vibaya fedha za umma.

Ndalichako alizungumzia hoja ya CAG kuhusu ukusanyaji hafifu wa fedha za mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu na akasema tangu serikali ya awamu ya tano iingie madarakani, kumekuwa na ongezeko la ukusanyaji wa madeni hayo.

"Taarifa ya CAG 2015/16 hadi 2016/17 inaonesha kuwa makusanyo yameongezeka kutoka Shilingi bilioni 8 hadi bilioni 116.  Hilo ni ongezeko la asilimia 300. Takwimu hazidanganyi," amesema.

Hata hivyo amesema bado makusanyo hayo hayatoshelezi na ameitaka Menejimenti ya Bodi ya Mikopo kuhakikisha ukusanyaji wa mikopo unaimarishwa.


No comments: