Wednesday, August 24, 2016

MR BLUE SI SHWARI, MKE WAKE ATUPA JIWE GIZANI

Mr. Blue "Baisa"akiwa na mkewe Warda siku ya ndoa yao.
Baada ya kuibuka kwa madai ya kuwa Mr Blue na Ex wake wa zamani Naj huwenda wakawa wanawasiliana, kumekuwa na vijembe vya maneno kutoka kwenye kambi ya Mr Blue ambavo vinahisiwa huwenda vikawa vinaelekezwa katika kambi ya Barakah Da Prince na Naj.

 Ilo limeibuka baada ya kipindi cha U-Heard cha Clouds FM kudai Barakah Da Prince ambaye ni mpenzi wa Naj, wiki chache zilizopita akiwa ameshika simu ya mpenzi wake huyo, alipiga mtu ambaye namba yake ‘iliseviwa’ Zai na baada ya Barakah kupokea alikuta sio mwanamke bali ni mwanaume ambaye alidaiwa kuwa ni Mr Blue.

Sakata hilo linadaiwa kuitikisa kambi ya Mr Blue, ambapo wiki hii rapper huyo alipost picha ya mke wake aitwae Walda na kuandika ujumbe wa kumfariji mpenzi wake huyo.

“Hakuna zaidi yako ndo maana nimekuoa,” aliandika Mr Blue kupitia instagram yake.

Baada ya kauli hiyo, Ijumaa hii mke wa Mr Blue ameonyesha kuguzwa na mambo yanayoendelea katika mitandao ya kijamii na kuamua kufunguka.

“Mke na mume hatutoi kiki endelea kuhangaika @mrbluebyser1988,” aliandika Walda instagram katika picha akiwa na mume wake.

Hata hivyo kambi ya Barakah Da Prince na Naj inaonyesha iko sawa kwani wawili hao wanaonekana kuwa na furaha.
Chanzo: Edwinmoshi Blog

No comments: