Saturday, August 17, 2013

FILAMU YA "FOOLISH AGE" YA LULU KUZINDULIWA 30 AGOSTI NDANI YA MLIMANI CITY


MSANII mwenye kipaji cha hali ya juu nchini na mwenye umri mdogo, Elizabeth Michael "LULU" anatarajia kuzindua filamu yake ya kwanza toka alipotoka gerezani, iitwayo "Foolish Age".

Filamu hii imetengenezwa na kampuni ya Proin Promotions Limited na itazinduliwa mnamo tarehe 30 Agosti 2013 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Filamu hiyo inayoelezea maisha ya Lulu ni moja ya filamu nzuri na yenye ubora wa hali ya juu kutokana na kutengenezwa na kampuni ya mahiri ya Proin Promotions Limited.

Katika uzinduzi huo, wasanii mbalimbali wakiwemo mwanamuziki Lady Jaydee na bendi yake ya Machozi anatarajiwa kushusha bonge la burudani siku hiyo.

Kupitia mtandao wa kijamii, Lulu aliandika "Nina kila sababu ya kumshukuru Mungu....!! nina furaha ya kuwafahamisha kuwa tarehe  30/08/2013 ndio siku nitakayozindua movie yangu mpya iitwayo FOOLISH AGE..... Hatimaye narudi kazini!!! Uzinduzi utafanyika katika ukumbi wa MLIMANI CITY..... kutakuwepo na wasanii mbalimbali wa muziki..... na pia LADY JAYDEE pamoja na MACHOZI BAND atakuwepo pia!!! nahitaji support ya mashabiki wote wa LULU na mashabiki wa BONGO MOVIE.....*PROINPROMOTERS"

Baada ya uzinduzi wa Filamu hii nakala zitaendelea kuuzwa katika maduka yote ya filamu nchini.  Filamu hii imetengenezwa na itasambazwa na kampuni ya Proin Promotions Limited.

Usikose uzinduzi huu utakaofanyika ndani ya ukumbi wa Mlimani City tarehe 30 Agosti 2013.

No comments: