Thursday, March 15, 2018

KAJALA AKANUSHA KURUDIANA NA P FUNK

Image result for picha za kajala masanja
Kajala Masanja.
STAA wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja ‘Kay’, amekanusha vikali madai ya kurudiana na baba mtoto wake, prodyuza Paul Matthyasse ‘P Funk’.

Madai hayo yalikuja hivi karibuni baada mwanamama huyo kutupia kipande cha video katika mtandao wa Snapchat kinachomuonesha akiwa na P Funk.
Image result for picha za kajala masanja
P Funk akiwa na mwanae, Paula.
“Jamani siwezi kurudiana na P, yule atabaki tu kuwa mzazi mwenzangu. Hiyo video tulikuwa tumekwenda shule kumwona mwanetu, Paula, baada ya hapo kila mtu alichukua hamsini zake,” alisema Kajala aliyezaa mtoto huyo mmoja wa kike na P Funk.

No comments: