Thursday, April 5, 2018

ABDUL NONDO AHOJIWA NA UHAMIAJI KUHUSU URAIA WAKE (Angalia VIDEO)


Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo ameitwa katika ofisi za Idara ya Uhamiaji ili kuhojiwa kuhusiana na uraia wake.

Nondo amefika ofisini hapo jana Aprili 4, 2018 kuitikia wito huo ambapo ameelezwa kuwa taarifa zake za uraia zinahitajika ikiwa ni pamoja na taarifa za wazazi wake na babu na bibi zake kwa pande zote mbili.

Ofisi hiyo ya Uhamiaji imemtaka Nondo kupeleka cheti chake cha kuzaliwa pamoja na vyeti vya wazazi wake wote wawili, babu na bibi zake hadi kufikia Aprili 20, 2018.

No comments: