Friday, February 16, 2018

MTOTO WA MIAKA 2 ARUDISHWA NCHINI BAADA YA WAZAZI KUKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA CHINA.... ANGALIA VIDEO

index
DAR ES SALAAM.  Mtoto mmoja wa kitanzania jana jioni amerudishwa nchini baada wazazi wake kuhukumiwa kifo nchini China kwa kosa la kukutwa na madawa ya kulevya.

Wazazi hao ambao ni watanzania, Baraka Malali na mkewe Ashura Mussa walikamatwa nchini China Januari 19 mwaka huu kwenye uwanja wa ndege wa Baiyun Guangzhou, wakiwa wamemeza tumboni dawa za kulevya na baada ya kuhifadhiwa kwenye chumba maalum kwa muda Baraka alitoa pipi 47 kwa njia ya haja ambapo mkewe alitoa pipi 82.

Watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa wameambatana na mtoto wao wa kike mwenye umri wa miaka 2 na miezi 9. Serikali ya China iliwasiliana na serikali ya Tanzania kuhusiana na suala la mtoto huyo ambapo walikubaliana kumrudisha mtoto huyo nchini ambapo mtoto huyo aliwasili nchini jana saa saba mchana akiwa ameambatana na Afisa wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi, Afrika Mashariki na Ushirikiano wa Kikanda.

Serikali kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Madawa ya Kulevya na Ustawi wa Jamii inafanya jitihada za kuwasiliana na ndugu na jamaa wa watuhumiwa ili kuhakikisha mtoto huyo anakabidhiwa kwao kwa ajili ya malezi na matunzo.

Taarifa Na: Rogers W. Siyanga Kamishna Jenerali: Mamlaka Ya Kudhibiti Na Kupambana Na Dawa Za Kulevya Nchini



No comments: