Thursday, April 19, 2018

KESI YA NONDO KUSIKILIZWA LEO 19 APRILI 2018

Kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP) na Mwanafunzi wa UDSM Abdul Nondo ambayo ilipaswa kusikilizwa kwa siku mbili mfululizo kuanzia jana Aprili 18, 2018 iliahirishwa mpaka leo kutokana na Hakimu wa kesi hiyo kuwa na kesi nyingi.

Mmoja wa mawakili wa Nondo wakili Chance Mloga amesema kuwa Hakimu John Mpitanjia jana aliomba kupumzika kutokana na uwingi wa kesi alizozisikiliza siku hiyo.

Wakili huyo amesema kuwa wamekubaliana kesi hiyo kusikilizwa tena leo mapema asubuhi huku upande wa Jamhuri tayari ukiwa umeleta mashahidi wanne wa kesi hiyo.

Nondo anatuhumiwa kwa makosa mawili; Kosa la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni Machi 7, 2018 akiwa Ubungo na kusambaza kwa kutumia mtandao wa WhatsApp kuwa yupo hatarini.

Shtaka la pili ni kutoa taarifa za uongo kwa watumishi wa umma mjini Mafinga alipokuwa akitoa taarifa katika kituo cha Polisi Mafinga kuwa alitekwa na watu wasiojulikana jijini Dar es Salaam na kupelekwa Kiwanda cha Pareto cha Mafinga.

No comments: