Friday, May 26, 2017

WOLPER ANG'AKA KUHUSIANA NA MADAI YA KUNUKA MWILI

Staa wa filamu ‘grade one,’ ‘Jacqueline Wolper’ ametokwa povu si la nchi hii baada ya kubanwa kuhusiana na madai ya kunuka mwili na kusema hajawahi kunuka maishani mwake na kwamba ingekuwa hivyo asingepapatikiwa na wanaume.

Wolper aliyaongea hayo hivi karibuni katika kipindi cha Shilawadu alipokuwa akihojiwa na mtangazaji wa runinga, Kwisa wa Kipindi cha SHILAWADU kinachorushwa na runinga ya Clouds.

Katika kuonesha kumaindi ile mbaya kuhusu madaia hayo, mrembo huyo ambaye kiukweli yuko bomba kwa muonekano alifunguka: “Aliyekuambia nanuka nani? Mimi sinuki wala sijawahi kunuka maishani mwangu, kuthibitisha hilo kwanza nisingekuwa napapatikiwa na wanaume kila kukicha sambamba na kuhongwa vitu kibao huku wengine nikiwaacha wakinililia.

Hao wanaosema na kusambaza hayo ni njia tu ya kujipatia followers kwenye mitandao yao kupitia mimi.” Wolper hakuishia hapo aliendelea kumwaga povu kuwa, tangu afungue duka la nguo ambalo amewekeza zaidi ya shilingi milioni 60, watu wengi wamekuwa wakichukizwa na maendeleo hayo. “Wana chuki tu na mimi, tangu nimefungua duka wananichokonoa, wanalishadadia hili jambo kisa tu nimepata mafanikio ya kufungua duka,” alipigilia msumari.
Chanzo: Ijumaa

Majina ya Wanafunzi wa Kidato cha Sita Waliochaguliwa Kujiunga na JKT 2017

TAARIFA KWA UMMA
Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), limechagua vijana waliohitimu Elimu ya Sekondari Kidato cha Sita kwa mwaka 2017, kutoka Shule zote za Tanzania Bara kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria.

BONYEZA HAPA KUONA MAJINA

Thursday, May 25, 2017

TANZIA: Mume wa Zari, Ivan Semwanga Afariki Dunia Leo


Aliyekuwa mume wa Zarina Hassan ‘Zari The Bosslady’, Ivan Semwanga (39) amefariki dunia akiwa hospitali nchini Uganda alipokuwa amelazwa kutokana na matatizo ya moyo usiku wa kuamkia leo Mei 25, 2017.

Ivan, aliyekuwa baba wa watoto watatu wa kiume wa Zari, aliachana na mwanamama huyo miaka michache iliyopita ambapo Zari alihamishia mapenzi kwa mwanamuziki Diamond Platinumz ambaye mpaka sasa wamezaa  watoto wawili, wa kike mmoja na wa kiume mmoja.

Ivan alikuwa maarufu Afrika Mashariki kutokana na biashara zake kubwa alizokuwa akifanya zikiwemo umiliki wa vyuo mbali mbali nchini Afrika Kusini.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Zari ameandika yafuatayo:
Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu Ivan Semwanga. Amina.