Wednesday, February 24, 2016

GARDNER: NDOA YANGU NA JAYDEE ILIVUNJWA KWA SIMU

jidenagardner
DAR ES SALAAM: Mtangazaji nyota wa redio nchini, Gardner G. Habash ambaye hivi karibuni aliachana rasmi na mkewe Lady Jaydee (Judith Wambura Mbibo) kwa talaka iliyotolewa mahakamani, amesema ndoa yake ilivunjika kwa kupigiwa simu ikitokea nchini Marekani.

Katika mahojiano maalum yaliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam, Gardner alisema hata hivyo, licha ya kutengana kwao, yeye hana chuki na mwanamke huyo aliyeishi naye takriban miaka kumi mfululizo.

Yafuatayo ni mahojiano kamili:

RISASI: Kuna uhusiano gani kati yako na Jide (Lady Jaydee) baada ya kutengana?

GARDNER: Hakuna tunapokutana wala hatuna mawasiliano, kwa hiyo hatuna uhusiano japo mimi sina tatizo lolote wala uadui na yeye, hata hivyo sitashangaa yeye kuonyesha uadui maana ilivyotokea hivyo miezi kadhaa iliyopita.

RISASI: Miezi kadhaa iliyopita kilitokea nini unachotafsiri kama uadui?

GARDNER: Niliona dalili ya chuki wakati fulani nilimshauri tutoe tamko la pamoja kuhusu kutengana kwetu, sababu watu walikuwa wanatuuliza maana hawakutuona pamoja, hakukubali na akataka niwe nasema tu siyo kweli ni uzushi, tuko pamoja japo hatukuwa pamoja hivyo kwa ujinga wangu nilikubali na ndiyo maana nilikuwa najibu watu kuwa sio kweli.

Sasa siku niliyoshtuka ni kwamba mimi nilikuwa nazifuata akaunti zake za mitandao kama mtu niliyekuwa nasimamia kazi zake na niliendelea hivyo miezi kadhaa baada ya kutengana, kwanza nikaambiwa ameenda redioni kutangaza kuwa ameniacha huku mimi ameniambia niseme tu kuwa siyo kweli, ikawa aibu kwangu.

Halafu baadaye nikaona katika mtandao wake kaongea vitu ambavyo aliweka kama anajibu maswali aliyoruhusu aulizwe, lakini kwangu mimi ilikua shambulio, ndipo nilipotafsiri kuna chuki lakini mimi sitamchukia wala siyo adui yake. Kwa sasa ninashukuru talaka imepatikana na najua huu sio mwisho wa kupenda.

RISASI: Hivi ni nini hasa chanzo cha kuvunjika kwa ndoa yenu?

GARDNER: Chanzo anaweza kukisema yeye aliyekataa kuendelea na ndoa, mimi sikuwa na tatizo na yeye, ijapokuwa kutofautiana kwa hapa na pale katika ndoa ni jambo la kawaida, lakini sijajua hadi leo kipi kipya kizito kilifanya yeye atake kutengana.

RISASI: Kwani ilikuwajekuwaje sasa?

GARDNER: Nakumbuka ilikuwa Julai 2014, nilipata booking ya show yake aende kuimba Marekani, ilikuwa ni safari ambayo ingedumu kwa siku saba, lakini mimi nikamshauri akae mwezi mzima yaani aongeze wiki tatu zaidi baada ya show ili iwe ni likizo yake. Basi ilipofika wiki ya tatu ya mwezi huo, ndiyo akanipigia kuniambia akirudi hataki tena kuendelea kuwa katika ndoa.

RISASI: Ulijisikiaje baada ya kupata ujumbe huo?

GARDNER: Kibinadamu mtu umekaa naye miaka mingi ghafla akiwa safarini anakutaarifu kuwa hataki muwe wote tena wakati kaondoka mko sawa, na jana yake mmeendelea kuweka mipango ya maendeleo, nilijisikia vibaya na nilijaribu kutafuta maongezi, alikataa na hakurudi tena nyumbani, ikabidi kukubali ingawa kishingo upande. Nashukuru Mungu nikaanza upya nikaona maisha mapya.

RISASI: Unaweza kusema wakati unakutana na Jide ulimkuta akiwa na nini na wakati mnaachana ulimuacha na nini?

GARDNER: Si uungwana mimi kutangaza nilimkuta na nini labda aseme yeye, lakini tulizalisha mali za kutosha, tulikuwa na vyanzo kadhaa vya fedha na kwa bahati nzuri wewe ulikuwa karibu nasi uliona na wengi waliokuwa jirani nasi wanajua. Mimi nimelelewa kushirikiana na kushea na kamwe siyo kunyang’anyana, ndiyo maana sitasema mambo ya mali, kama kipo ninachostahili nt’akipata tu.

Ijapokuwa yeye amekuwa akipotosha watu kuwa mimi sikuwa na kitu, sikuwa na mchango wa kipato wala wa taaluma katika muda tuliokaa pamoja yaani ni kama Mario ninayemtumia na nilisikitika zaidi pale mahakamani Sinza hakimu alipomuuliza, ninanukuu ‘Kuna mali zozote mlipata wakati mko pamoja katika ndoa,? Yeye akajibu hamna. Hata hivyo mimi sijawahi kuonesha hata nia ya kutaka tugombee mali, nilimpa yeye aamue kila kitu ili kuepuka kulumbana lakini baadaye nikalipuliwa, hahahaha, najua mengi yatasemwa nipakwe ubaya.

Baada ya mahojiano hayo mafupi, gazeti hili lilimtafuta Jaydee na kufanikiwa kumpata kupitia simu yake ya mkononi.

RISASI: Mambo sista?

JAYDEE: Poa, nambie

RISASI: Mashabiki wa kapo yenu wangependa kujua nini hasa kilitokea katika ndoa yenu.

JAYDEE: Hivi stori moja mnaandika mwaka mzima? Kuna kipya gani hapo ambacho hamjaandika? Halafu kulikuwa na mashabiki wa Jaydee, hakukuwa na mashabiki wa couple.

JAYDEE: Hebu kuwa positive, kuna vitu vingi vizuri vya kuandika kuhusu mimi.
Chanzo: Global Publishers

Monday, February 22, 2016

LULU AONGEA BAADA YA KUZUSHIWA KIFO

Elizabeth Michael ‘Lulu’ ni staa kutoka kiwanda cha filamu Tanzania, hivi leo Feb 22 amezichukua headline kwa kuandika yafuatayo kupita mtandao wake wa instagram kuhusu kuzushiwa kifo.

"Nasikia nimekufa wewe uliyepost  hii kama wewe utakwepo tutaonana tena 2017 inshaalah alafu jifunze na kuandika ELIZABETH vizuri Kwanza (niki repot LIVE kutoka heaven) this shows jina langu lina KIKI nishasema mniache jmn watsup Kufa nitakufa sikatai lkn mpk nimalize miaka iliyoandikwa kwenye Biblia."
 
elizabeth
elizabethmichaelofficial  Nasikia Nimekufa 💃💃💃💃💃💃
Wewe uliyePost hii😷😷😷Kama wewe utakuwepo TUTAONANA TENA 2017 Inshaallah
Alafu jifunze na kuandika ELIZABETH vizuri kwanza.....
(Niki report LIVE kutoka heaven)💃
This shows how Jina Langu lina KiKi😋nishasema MNIACHE JMN😪watsup!???😳
Kufa ntakufa SIKATAI lkn mpk nimalize MIAKA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA😎
Chanzo:  Millard Ayo.com

WASANII WAWILI WAFA BONGO MUVI

BACK-WIKIENDA
Stori: Imelda Mtema, Wikienda
Dar es Salaam: Misiba! Wakati wadau wa Bongo Movies wakiwa kwenye majonzi ya kifo cha Michael Dennis ‘John Woka’, kwenye Bongo nako kuna pigo la kuondokewa na wasanii wawili, Maneno Gongo ‘Mr Gongo’ na Jennifer Vincent ‘Mama Utajiju’.

Gongo alifariki dunia wiki iliyopita katika Hospitali ya Muhimbili baada ya kusumbuliwa na presha kwa muda mrefu.
BACK-WIKIeENDA
Marehemu Gongo, enzi za uhai wake.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda kwa masikitiko, ndugu wa marehemu Gongo aitwaye Hamza Mchuwa, alisema kuwa msanii huyo alisumbuliwa na maradhi hayo kwa muda refu na alikuwa akijaribu kila dawa bila mafanikio.

Mchuwa alisema kuwa jamaa huyo alizidiwa hadi akakakamaa hivyo walimpeleka Muhimbili ambapo ndiko alikokutwa na umahuti.

Msanii huyo ambaye alizikwa kwenye Makaburi ya Visiga, Kibaha mkoani Pwani amecheza filamu mbalimbali zikiwemo The Mask akiwa na Aunt Ezekiel, For Sale, Stolen Gold, Sara na nyinginezo.
Wakati simanzi hiyo haijapoa, mwigizaji mwingine, Mama Utajiju yeye aliaga dunia kwa kuumwa ghafla.

“Nasikitika kuondokewa na msanii wangu mzuri kama mtakumbuka alifanya vizuri sana kwenye Filamu za Mwanavita, Nakufa kwa Ajili Yako na Yote ni Baba,” alisema mkurugenzi wa kundi hilo, Fatma Makame ‘Joanitha.
Chanzo: Global Publishers

RAY C AFUNGIWA HOSPITALINI

ray-c1 (1)
Mwanamuziki wa bongo fleva, Rehema Chalamila a.k.a. Ray C.
Dar es Salaam: Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ anadaiwa kuwekwa chini ya uangalizi maalum akiwa amefungiwa kwenye Hosptali ya Mwanayamala, Dar baada ya madai ya kurudia matumizi ya madawa ya kulevya ‘unga’.

Chanzo makini cha Ijumaa Wikienda kilimshuhudia Ray C akiwa kwenye wodi maalum ya waathirika wa unga huku mama yake mzazi akiwa anamuangalia wakati wote.

Mpashaji wetu huyo alifunguka kuwa, kuna muda Ray C alitoka nje na kuanza kuongea maneno ambayo hayajanyooka lakini dakika chache baadaye alikuja muuguzi na kuanza kumtafuta kwa kumuita jina lake akihofia huenda ametoka nje ya geti.
FRONT WIKIENDA2 copy
Chumba kilichopo hospitali ya Mwananyamala ambacho inasemekana ndipo Ray C alipofungiwa kwa matibabu.

“Jamani Ray C yupo hapa, anaonekana hayuko sawa kabisa kwa sababu ametoka hapa nje ya wodi ameanza kuzungumza vitu ambavyo havieleweki,” kilisema chanzo hicho.

Kilizidi kuweka wazi kuwa baadhi ya waathirika wenzake walikuwa wakimsema kuwa bado ameweka ustaa mbele, kitu ambacho kinamuharibia kwa kuwa hafuati masharti ya kutumia dozi hiyo ya kuacha unga ya Methadone.

Gazeti hili lilifunga safari hadi hospitalini hapa ambapo lilionana na daktari wa kitengo hicho (jina tunalo) ambaye alikiri kuwa mwanamuziki huyo yupo hospitalini hapo kwa matibabu.

“Kuna hali fulani inawapata sana wagonjwa wetu maana wanahitaji sana utulivu hivyo yuko hapa kwa ajili ya tiba na muda si mrefu atakuwa tena uraiani kama zamani, tunajitahidi kumtibu ili awe sawa,” alisema daktari huyo.
Chanzo: Global Publishers